Kwa muonekano hali ya sasa ya dunia imekuwa tete kulingana na mabadiliko ya hali ya hewa ongezeko la watu.pamoja na shughuli za kiuchumi zinazofanyika na binadamu
Miongoni mwa shughuli za kibinadamu zinazochangia uharibifu wa mazingira tumejumuisha baadhi ya shughuli hizo ni
Kilimo; ni shughuli ya uzalishaji mali ambapo ardhi hutumika kama msingi mkuu wa uzalishaji katika kilimo uharibifu wa mazingira hutokea kwakuwa ardhi huitajika kwaajili ya shughuli hiyo..hivyo basi wanadamu hufyeka misitu ili kupata maeneo ya kulimia na mwisho wa yote ardhi hubaki kame na kusababisha uharibifu wa mazingira
Ufugaji;Hii ni shughuli ya kiuchumi inayofanyika kwa kufuga mifugo ili kujiongezea kipato.shughuli ya kilimo pia huweza kuchangia uharibifu wa mazingira kwa baadhi ya wafugaji kufuga mifugo mingi katika eneo dogo kuthibiti hili
Tunashauriwa kufuga mifugo michache katika eneo husika ,kufuata njia za kisasa za ufugaji ambao pia ufugaji wa kisasa unatija kwa mfugaji
Ongezeko la watu;Ongezeko la watu pia huchochea uharibifu wa mazingira kutokana na watu kuhitaji maeneo kwajili ya kujenga,kuzalisha mali na mambo mengine mengi.ongezeko la watu kwa sasa linachochewa na kutokuwa na njia thabiti ya kithibiti uzalianaji holela bila kufuata mpango wa uzazi.
Uthibiti hili kulithibiti watu wanapaswa kufuata njia za kisasa za uzazi wa mpango kizui uzalianaji holela...
Hizo ni baadhi ya sababu zinazochochea uharibifu wa mazingira
Tunaipenda dunia kuitunza
Katika maandiko Mungu anatuambia nimewapa mamlaka mkatawale na kumiliki.vyote tulivyopewa tumepewa tuvitunze na siyo kuharibi
Sawa tufanyaje kuthibiti hili
1>tusikate miti hovyo ,
2>Tuoteshe miti kiweka hali ya ukijani kila wakati
3>Tusambaze elimu juu ya utiunzaji wa mazingira
4>Tupunguze matumizi ya nishati inayochochea uharibifu wa mazingira kama mkaa, na kuni badalayake tutumie nishati jadidifu na rafiki kwa mazingira kama gesi na umeme
5>tutizame kesho yetu na kizazi chetu cha baadae kwa lengo la kukiwekea mazingira bora yatakayowafanya waishi bila changamoto
Ahsante kubwa
Mick Daniel/Abdallah A Shaban



Comments
Post a Comment